Saturday, September 8, 2012

RAIS KIKWETE AUDHURIA MKUTANO WA VIONGOZI WA MAZIWA MAKUU, KAMPALA





Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika Mkutano wa Viongozi wa nchi za Maziwa Makuu wanaokutana katika ukumbi wa mikutano wa Munyonyo Commonwealth Resort jijini Kampala leo Septemba 8, 2012 


Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taif Mhe. Shamsi Vuai Nahodha (kulia kwake) na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Balozi Rajab Gamaha wakielekea kwenye mkutano wa viongozi wa nchi za Maziwa Makuu wanaokutana katika ukumbi wa mikutano wa Munyonyo Commonwealth Resort jijini Kampala leo Septemba 8, 2012

PICHA NA IKULU

Wednesday, September 5, 2012

MKUTANO WA ASASI YA SIASA, ULINZI NA USALAMA YA JUMUIYA YA MAENDELEO YA NCHI YA KUSINI MWA AFRIKA (SADC TROIKA)






Katibu Mtendaji wa SADC  Dkt Tomaz A. Salomao akitoa maelezo kabla ya kuanza kikao


Maofisa wakimsikiliza Mwenyekiti wa Asasi ya Siasa, Ulinzi na Usalama ya Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi ya Kusini mwa Afrika(SADC TROIKA) Rais Jakaya Kikwete akifungua kikao cha siku moja cha asasi hiyo katika hoteli ya Kilimanjaro Hyatt Regency jijini Dar es salaam




Kuanza kwa kikao cha Asasi ya Siasa, Ulinzi na Usalama ya Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi ya Kusini mwa Afrika(SADC TROIKA).


Mwenyekiti wa Asasi ya Siasa, Ulinzi na Usalama ya Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi ya Kusini mwa Afrika(SADC TROIKA) Rais Jakaya Kikwete akiongea na wanbahabri mara baada ya kumalizika kikao cha siku moja cha asasi hiyo katika hoteli ya Kilimanjaro Hyatt Regency jijini Dar es salaam. Kushoto ni Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mhe. Bernard Membe na kulia ni Katibu Mtendaji wa SADC  Dkt Tomaz A. Salomao


Mwenyekiti wa Asasi ya Siasa, Ulinzi na Usalama ya Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi ya Kusini mwa Afrika(SADC TROIKA) Rais Jakaya Kikwete akiwa na wageni wake wakielekea kwenye  kikao cha siku moja cha asasi hiyo katika hoteli ya Kilimanjaro Hyatt Regency jijini Dar es salaam. Kutoka kushoto ni Rais Hifikepunye Pohamba  wa Namibia, Rais Kikwete, Rais Armando Emílio Guebuza wa Msumbiji na Rais Joseph Kabila wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC)

PICHA NA IKULU

Saturday, September 1, 2012

VODACOM YACHANGIA MRADI WA KUHIFADHI MBWA MWITU HIFADHI YA SERENGETI

Mbwa mwitu wakila nyama
Rais Jakaya Mrisho Kikwete ameishukuru kampuni ya simu za mkononi ya Vodacom kwa kuchangia katika mradi wa kuhifadhi mbwa mwitu katika hifadhi ya Taifa ya Serengeti, mradi unaojulikana kama Vodacom Foundation Serengeti Wild Dogs Conservation Project, kwa dola za Marekani 450,000 kwa kipindi cha miaka mitatu.

Rais ametoa shukrani hizo Kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Vodacom hapa nchini Bw. Rene Meza, Ikulu Dar-Es-Salaam, walipokutana jana jioni, Ijumaa Agosti 31,2012

"Napenda kutoa shukrani zangu kwa Vodacom kwa msaada huu mkubwa, tunashukuru kwa jitihada zenu kubwa katika hili" Rais amesema.

Naye Mtendaji Mkuu wa Vodacom amemhakikishia Rais kuwa kampuni yake itaendelea kushirikiana na serikali katika miradi mbalimbali ya maendeleo, elimu na Afya.

“Tunajisikia faraja sana kuwa miongoni mwa washirika wa mradi huu. Ni heshima kwetu na tuko makini nao, tunataka kuendelea na mradi huu" Bw, Rene Meza amemhakikishia Rais.

Tayari mbwa mwitu kumi na Moja, wamerudishwa mbugani siku ya Alhamisi Agosti 30, 2012 baada ya kuhifadhiwa kwenye boma maalumu la mradi huo, katika eneo la Nyamuma, Magharibi mwa Hifadhi ya Taifa ya Serengeti, mkoani Mara.

Wadau wengine walioshiriki na kufanikisha zoezi hilo ni pamoja na Idara ya Wanyamapori, Mamlaka ya Hifadhi za Taifa (TANAPA), Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro (NCCA), Frankfurt Zoological Society, Grumeti Fund na Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro.

Kuachiwa kwa Mbwa Mwitu hao 11 walioondolewa katika msitu wa Samunge wilayani Loliondo ni mojawapo ya juhudi za kurudisha tena makundi ya wanyama hao katika mbuga hiyo maarufu duniani. Hivi sasa kuna makundi 11 yanayofuatiliwa, manane yakiwa Loliondo na matatu katika Hifadhi ya Ngorongoro, yakifanya jumla ya Mbwa Mwitu 200.

Mtafiti wa Magonjwa ya Wanyama kutoka Taasisi ya Utafiti wa Wanyama (TAWIRI) Dkt. Ernest Mjingo, alimwambia Rais Kikwete kwamba katika Hifadhi ya Serengeti makundi ya Mbwa Mwitu yalikuwa yakionekana kwa wingi, lakini sasa yametoweka na mara ya mwisho Mbwa Mwitu wawili walionekana mwaka 1998.

Mtafiti huyo alisema Mbwa Mwitu wamekuwa wakitoweka kutokana na kuuawa kwa sumu na wananchi baada ya kula mifugo yao na kuugua magonjwa mbalimbali kama kichaa cha mbwa.

Dkt. Mjingo alisema baada ya kuachiwa Mbwa Mwitu hao, waliovishwa collar maalumu zenye redio, juhudi zitaendelea ili kupata makundi sita yenye Mbwa Mwitu takriban kumi kila moja, ikiwa ni hatua endelevu ya muda mrefu ya kuhakikisha uwepo wa wanyama hao mbugani humo.

Mbwa Mwitu ni miongoni mwa wanyamapori ambao wapo hatarini kutoweka duniani. Takwimu zinaonyesha kuwa katika Bara la Afrika kuna Mbwa Mwitu wanaofikia 8,000 na Tanzania pekee inakadiriwa kuwa wanyama hao 3,500 katika mbuga mbalimbali nchini. Katika Hifadhi ya Taifa ya Serengeti walitoweka kabisa kabla ya juhudi hizi za kuwarejesha kuanza. 




 

Wednesday, August 29, 2012

BODABODA YAUA 251 NDANI YA MIEZI MITATU

Madereva wa bodaboda wakisubiri abiria huku wamelala
Na Dennis Mwasalanga

Jumla ya watu 251 wameuwawa katika ajali zilizohusisha usafiri wa Bodaboda jijini Dar es salaam katika kipindi cha miezi mitatu iliyopita jijini.



Katika ajali hizo zaidi ya watu 1289 wamepata majeraha huku wengine wakipata ulemavu wa kudumu.


Wadau wa Usalama barabarani wameainisha kuwa, biashara holela kwa madereva wasio na mafunzo NI chanzo cha ongezeko la ajali vyombo hivyo vilivyoshika kasi kipindi cha hivi karibuni.

Baadhi ya waendesha vyombo hivyo vya usafiri wamekana kuwa wao pekee ndo chanzo cha ajali bali ni kukosekana kwa umakini baina ya mamlaka za usalama pamoja na wamiliki wa vyombo vya usafiri

Kamanda poilisi kikosi cha usalama barabarani kamanda Mohammed Mpinga, ikiwa ni moja ya mbinu za kukabiliana na ajali kwa kushirikiana na wadau wa vyombo vya usafiri wamekuatana jijini Dar es salaam na kuzindua mafunzo kwa madereva zaidi ya elfu moja yatakayotolewa bure kwa yeyote aliye na nia ya kuwa dereva bora wa bajaji na bodaboda jijini hapa.

Kwa upande mwingine wizara ya mambo ya ndani bado ina kazi kubwa ya kufanya kwenye upenyo wa biashara huria na bado kuna mwanya wa uzembe katika kusimamia kiuhakika usalama wa vyombo vya usafiri, Nizar Jivani ni Rais wa chama cha wamiliki wa bodaboda na bajaji AAT.

Ajali za barabarani licha ya maangalizo mbalimbali yanayoatolewa zimeendelea kuwa wimbo wa kila uchao huku maisha ya wananchi yakiendelea kuteketea, na kubwa ikiwa ni ongezeko la kizazi tegemezi kutokana na wengi kuachwa wakiwa na ulemavu .

Tuesday, August 28, 2012

INDIA KULETA WATAALAM WA AFYA KUTOA HUDUMA KWA BEI NAFUU

Na Joyce Mwakalinga

Ubalozi wa India nchini Tanzania unatarajia kuleta wataalamu wa afya Tanzania kutoka hospitali kubwa nchini India watakaotoa huduma za afya kwa bei nafuu.

Ugeni huo ulioandaliwa na taasisi ya shirikisho la biashara na maonyesho la nchini India IMTD utawasili jijini Dar Es Salaam mwishoni mwa mwezi huu.


Wataalamu hao wa afya kupitia shirika hilo la nchini india la Indian Medical Tourism Destination IMTD watatoa huduma hizo kupitia maonyesho yatakayofanyika jijini Dar es Salaam.

Mwakilishi wa ubalozi wa india Nchini Tanzania Debnath Shaw anasema hatua ya utoaji wa huduma hizo zitawasaidia watanzania wengi ambao wamekuwa wakifuata matibabu nchini mwao.

Naye mkurugenzi wa shirikisho la wafanyabiashara wa viwanda nchini India FICCI Vivek Kodikal anaelezea ni jinsi gani watanzania wanatumia gharama kubwa kwa kutibiwa India.

Maonyesho hayo yatarajiwa kufanyika katika ukumbi wa Diamond Jubilee kwa siku mbili mfululizo za Agost 30 na 31.

Watakaoshiriki ni pamoja na wataalamu mbalimbali wa afya kutoka nchini Tanzania, wadau katika sekta ya afya kutoka nchini india ambao ni pamoja na wawakilishi kutoka hospitali na vituo vikubwa vya afya.

Saturday, August 4, 2012

SERIKALI NA WADAU WA MAENDELEO WATAKIWA KUTOA KIPAUMBELE KWA VIJANA WENYE UJUZI NA VIPAJI

Serikali pamoja na wadau wa maendeleo nchini wametakiwa kutoa kipaumbele kwa vijana wenye ujuzi na vipaji mbalimbali ili kusaidia kuinua vipaji vyao na kujikwamua kiuchumi.
 Wito huo umekuja kufuatia kundi kubwa la vijana wanaomaliza kukosa ajira licha ya kuwa na vipaji kutokana na aidha kukosa fursa za kuajiriwa au mitaji ya kujiajiri wenyewe.

Mwenyekiti mtendaji wa kikundi cha vijana wajasiriamali Twisuka Bibi Mary Mkalawa amesema vijana wa Pwani wana moyo wa kujituma katika kujiendeleza kimaendeleo lakini wamekosa fursa ya kutumia vipaji vyao kwa kukosa mitaji, mikopo na Ruzuku toka serikalini.

Vijana hao wajasiriamali wamesema katika kipindi hiki cha mfungo wa Ramadhani soko limepungua kutokana na kukosekana kwa wageni .

Serikali pamoja na wadau wa maendeleo nchini wamekuwa wakiungana na makundi ya vijana katika kusaidia kupunguza tatizo kubwa la ukosefu wa ajira nchini.

MAHARAMIA WASHAMBULIA MELI ZA MAFUTA NCHINI NIGERIA


Watu wenye silaha wameshambulia meli mbili nje ya eneo la mafuta la Nigeria, eneo la mdomo wa Mto Niger.
 
Walinzi wawili waliuwawa na wawili kujeruhiwa katika shambulizi hilo.

Washambuliaji hao, ambao hawakujulikana, pia waliwateka nyara mabaharia wanne.

Jeshi la wanamaji la Nigeria nalo linashiriki kuwasaka washambuliaji hao.

Shambulio hilo limetokea siku tu baada ya serikali ya Nigeria kutangaza kuwa itatumia satalaiti kuzuwia magendo ya mafuta katika eneo hilo, ambayo huuzwa kwenye soko la kimataifa.