Serikali imetenga zaidi ya shilingi bilioni 400 kwa ajili ya kuziwezesha kaya masikini katika Wilaya tatu za Kibaha, Bagamoyo na Chamwino ikiwa ni awamu ya tatu ya utekelezaji wa mpango wa maendeleo unaosimamiwa na Mfuko wa maendeleo ya jamii Tanzania TASAF.
Mpango huo ambao ulianza kwa majaribio katika Wilaya hizo kuanzia mwaka 2005,unaelezwa kuleta mafanikio kutokana na kuziwezesha kaya masikini ambazo zinaongozwa na Wazee,watoto na wajane ambapo Fedha hizo zimetolewa kwa ushirikiano wa Bank ya Dunia,Shirika la maendeleo la Uingereza DFID na Serikali ya Hispania.


No comments:
Post a Comment