![]() |
| Geti la hospitali ya Muhimbili |
![]() |
| Baadhi ya wagonjwa wakisubiri huduma bila mafanikio |
![]() |
| Mmoja wa wagonjwa waliofika hospitalini hapo |
Siku moja baada ya Serikali kushindwa kutoa msimamo wake kuhusiana na mgomo wa madaktari unaoendelea nchi nzima utoaji wa huduma katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili umesimama kufuatia mgomo huo.
June 27, mwaka huu bungeni mjini Dodoma Waziri Mkuu Mizengo Pinda alitangaza kutoa tamko kuhusiana na mgomo huo siku inayofuatia ambapo hali ilikuwa tofauti baada ya msimamo huo kushindwa kutolewa.
Kufuatia hali hiyo baadhi ya wananchi na wagonjwa waliofika hospitalini hapo wameishauri serikali kukaa meza moja na madaktari ili kupata suluhisho la mgogoro huo kutokana na kuwaathiri watanzania wengi hususani wenye kipato cha chini.
Juni 21, mwaka huu Jumuiya ya Madaktari Tanzania ilitangaza kuanza kwa mgomo rasmi wa madaktari usio na kikomo nchi nzima hadi serikali itakapoanza kutatua madai yao yaliyowasilishwa serikalini Januari 27, mwaka huu ambapo miongoni mwa madai hayo ni pamoja na uboreshwaji wa mazingira ya kufanyia kazi na nyongeza ya posho na mishahara.




No comments:
Post a Comment