Chama cha netiboli nchini CHANETA kimezitaka timu mbalimbali zitakazoshiriki mashindano ya ligi daraja la kwanza kurudisha fomu za kushiriki ligi hiyo inayotarajiwa kuanza septemba 8 mwaka huu mjini Mbeya.
Kaimu katibu mkuu wa CHANETA Rose Mkisi amesema kuwa fomu hizo zinatakiwa kurudishwa kabla ya julai 30 mwaka huu ili kuwezesha kamati ya mashindano kukamilisha mapema mipango ya michuano hiyo.
Michuano hiyo inatarajiwa kushirikisha jumla ya timu 20 kutoka Tanzania bara na visiwani.
No comments:
Post a Comment